Kimbunga Nate chatua majimbo ya Louisiana na Mississippi nchini Marekani


A resident watches the rising waves in Masachapa beach during heavy rains due to Tropical Storm Nate in the city of Masachapa, about 60km from the city of Managua on October 5, 2017Haki miliki ya picha
Image captionUharibbifu nchini Nicaragua
Kimbunga Nate kimesababisha upepo mkali, mvua kubwa na mafuriko kwenye pwani ya Ghuba ya Marekani.
Kimbunga hicho chenye upepo unaovuma kwa kasi ya kilomita 137 kwa sasa, kilitua karibu na mto Mississipi huko Louisiana baada siku ya Jumamosi.
Kikisonga kwenda kaskazini kilitua eneo la Bioloxio huko Mississipi
Louisiana, Mississippi, Alabama na sehemu za jimbo la Florida mapema zilitoa onyo kuhama wakati kukiwa na hofu ya kuongezaka kwa haraka viwango vya maji.
Nate kiliwaua takriban watu 25 huko Nicaragua, Coasra Rica na Honduras.
People fill sandbags as they prepare for Hurricane Nate in New Orleans, 7 October 2017Haki miliki ya picha
Image captionWakaazi wa New Orleans wakijiandaa
Kimbunga hicho kisha kikaongeza nguvu hadi kiwango cha kwanza eneo la Saffir-Simpson scale kilipoelekea Marekani.
Wakati Nate kilisonga mbele mitaaa na barabara huko Biloxi vilifurika
Rais wa Marekani Donald Trump siku ya Jumamosi alitangaza hali ya dharura huko Louisiana, na kuruhusu jimbo hilo kuomba msaada wa serikali kwa maandalizi.
Huko Alabama, gavana wa Republican Kay Ivey, aliwashauri wakaazi katika sehemu zinazokumbwa na upepo mkali kuchukua tahadhari.
Bandari tano zilifungwa kama njia ya kuchukua tahadhari.
A man recovers some zinc sheets after a mudslide damaged their homes during heavy rains by Tropical Storm Nate in San Jose, Costa Rica October 5, 2017Haki miliki ya picha
Image captionCosta Rica ni kati ya nchi zilizopiwa na kimbunga hicho

Comments