NIKKI WA PILI ATUPA JIWE GIZANI

Image result for nikki wa pili
Msanii Nikki wa Pili ambaye ni miongoni mwa wasanii wachache wanaofanya uchambuzi wa masuala mbali mbali ikiwemo uchumi wa taifa, ametupa jiwe gizani kuhusu sera mpya ya viwanda.

Kupitia ukurasa wake wa twitter Nikki wa Pili ameandika ujumbe kuhusu sera mpya ya Tanzania ya viwanda inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano, na kusema kwamba ni vyema tukajitafakari kwa hili kwani nchi ambazo zimefanikiwa, zilitumia mfumo wa ruzuku na sio wawekezaji pekee.

"Kupitia ruzuku ya serikali, na ulinzi dhidi ya ushindani wa kisoko kwa miaka 40 ndipo Japan wakafanikiwa kuisimamisha secta ya viwanda vya magari, sasa tunao hubiri Tanzania ya viwanda kupitia wawekezaji na ushindani wa kisoko tujitafakari",ameandika Niki wa Pili.

Sasa hivi Tanzania inapambana kuleta mapinduzi ya viwanda ili nchi iweze kuzalisha vitu vingi yenyewe bila kuagiza nje, huku ikitoa fursa kwa wawekezaji mbali mbali kuja nchini kuwekeza kwenye sekta ya viwanda.

Comments